Straika wa Uingereza arudi kisa Samatta
Muktasari:
- Mchezaji huyo alisema kwamba aliongea na Samatta kuhusu kushiriki katika tukio hilo, ambapo aalipohakikishiwa aliamua kujiunga na nyota wenzake.
Dar es Salaam. Mshambuliaji Adi Yusuf anayekipiga katika kikosi cha Solihull Moors Fc kinachoshiriki Ligi Daraja Kwanza England amejikuta kuguswa na kitendo cha mshambuliaji Mbwana Samatta cha kuchangisha pesa kwaajili ya Shule za Msingi.
Mchezaji huyo alisema kwamba aliongea na Samatta kuhusu kushiriki katika tukio hilo, ambapo aalipohakikishiwa aliamua kujiunga na nyota wenzake.
"Niliongea na Samatta akanambia kwamba kuna kitu cha muhimu anakifanya kwahiyo nikaona nije, hapa unaponiona nina masaa matatu tangu nishuke katika Ndege ndio maana nimechelewa uwanjani hata kucheza pia," alisema.
Yusuph ambaye naye amekuwa akiendesha hisani yake ya kusaidia watoto na watu wasiojiweza, alisema anaendelea nayo na ana lengo la kuitanua zaidi.