Snura, Sultan King kuipamba Taifa Moja Iddi

Muktasari:

Pili kwenye viwanja vya  Mnazi Mmoja, Zanzibar 

Dar   es   Salaam. Mwanamuziki Snura na  Sultan  King  watatumbuiza katika tamasha la   kampeini  ya Taifa Moja litakalofanyika Zanzibar siku ya Iddi Pili kwenye Viwanja vya  Mnazi Mmoja.

Tamasha hilo linalengo ya kutoa elimu kwa Wananchi kupitia burudani juu ya uhuru wa kutuma pesa bila mipaka na ushirikiano wa makampuni matatu ya simu za  mkononi kupitiia huduma zao TigoPesa, Airtel Money na Ezy Pesa.

Mratibu wa tamasha hilo Mkurugenzi wa kampuni ya Fern Tanzania, Liginiku Millinga   alisema maandalizi yote yamekamilika na  kuwaomba wakazi wa Zanzibar kujitokeza kwa  wingi kupata burundani kutoka kwa  wasanii  hao pamoja na kupata elimu juu ya kutuma na kupokea pesa kwenda mtandao wowote hapa Tanzania kwa gharama ile ile.

Millinga alisema sasa ni zamu ya Zanzibar siku ya Iddi Pili kwenyeviwanja vya Mnazi Mmoja watashudia burudani kutoka kwa Snura  pamoja na Sultan  King.

"Tangu tuanze kampeni yetu ya Taifa Moja tumepata mafanikio mengi na kufikisha ujumbe wetu wa uhuru wa kutuma pesa bila mipaka kupitia burudani kutoka kwa wanamuziki mbalimbali," alisema Millinga.

Hayo makampuni ya simu za mkononi wameamua kuungana na taifa moja katika kutoa huduma ya kutuma na kupokea fedha.

Millinga aliongeza hali hii imewafanya Watanzania kutokuwa na wasiwasi tena pale anapotaka kutuma pesa kwani hanakuwa na uhuru wa kutuma pesa kwenda mtandaowowote kwa gharama ile ile.