Siri ya Azam FC kutofungwa hata bao moja hii hapa

Muktasari:

Azam na Simba ndio timu pekee ambazo hazijaruhusu nyavu zao kutikiswa kwenye mechi tatu za Ligi Kuu Bara msimu mpaka sasa.

Dar es Salaam. Beki wa Azam, Aggrey Morris amesema ubora, umoja na morali iliyopo katika safu yao ya ulinzi ndio siri ya kutoruhusu bao lolote mpaka sasa kwenye Ligi Kuu Bara msimu huu.
Azam na Simba ndio timu pekee ambazo hazijaruhusu nyavu zao kutikiswa kwenye mechi tatu za Ligi Kuu Bara msimu mpaka sasa.
Morris alisema wamejiwekea malengo msimu huu ya kuhakikisha wanaweka rekodi ya kuwa timu ambayo haijaruhusu bao msimu huu ingawa amekiri si kazi nyepesi lakini bidii na kujituma inawasaidia kutimiza malengo yao.
" Hakuna kingine kiinachoibeba safu yetu ya ulinzi kama umoja tulionao na kila mmoja kujua nini anatakiwa kufanya na kusaidiana.Hali hii imetufanya kutengeneza ukuta wa chuma ni ngumu kupitika kirahisi.