#WC2018: Senegal yabeba matumaini kutinga 16 bora

Muktasari:

  • Senegal na Japan ili kuwa na uhakika wa kufuzu hatua ya 16 bora zitasubiri matokeo ya mechi baiana ya Poland na Colombia mchezo unaotarajiwa kupigwa usiku huu leo Jumapili.

Timu za Senegal na Japan zimegawana pointi baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 huku sare hiyo ikiziweka kwenye matumaini ya kufuzu hatua ya 16 bora baada ya kufikisha pointi nne kila moja.

Senegal na Japan ili kuwa na uhakika wa kufuzu hatua ya 16 bora zitasubiri matokeo ya mechi baiana ya Poland na Colombia mchezo unaotarajiwa kupigwa usiku huu leo Jumapili.

Sare yoyote ya Poland na Colombia itakuwa imezipa nafuu Japan na Senegal na kuzipa nafasi ya kubwa ya kusonga mbele.

Kundi H ambalo lina timu za Japan, Senegal, Poland na Colombia zitakamilisha mchezo wa tatu kila moja Juni 28 ambapo Colombia itakutana na Senegal huku Japan wakiwavaa Poland.