Ni Okwi! Okwi! Okwi! Uwanja wa Kirumba Mwanza

Muktasari:

Aidha mashabiki hao mkoani hapa wameonyesha mapenzi makubwa kwa mchezaji huyo baada ya kununua kwa wingi jezi zenye namba ya Mganda huyo.

Mwanza. Mashabiki wa Klabu ya Simba wameshindwa kujizuia juu ya mapenzi yao kwa nyota wao, Emanuel Okwi baada ya kuingia uwanjani wakitaja jina la mshambuliaji huyo.
Aidha mashabiki hao mkoani hapa wameonyesha mapenzi makubwa kwa mchezaji huyo baada ya kununua kwa wingi jezi zenye namba ya Mganda huyo.
Awali, jana Jumatano mashabiki wengi walifurukia uwanjani hapo kutaka kumuona Okwi akifanya mazoezi na kikosi hicho jambo ambalo walikataliwa kutokana na kuwapo ulinzi mkali.