Msuva aipa matumaini ya ushindi Difaa
Muktasari:
Katika michuano hiyo ya Moroccan Throne Cup, Difaâ ilitoshana nguvu na Ittihad kwenye mchezo wa awali kwa kutoka sare ya bila kufungana.
Dar es Salaam. Timu ya Difaâ Hassani d'el-Jadida anayoichezea mshambuliaji wa Kitanzania Simon Msuva, inasafiri leo kutoka El Jadida kuelekea Tangier kucheza mchezo wa marudiano na Ittihad Tanger, Jumatano.
Katika michuano hiyo ya Moroccan Throne Cup, Difaâ ilitoshana nguvu na Ittihad kwenye mchezo wa awali kwa kutoka sare ya bila kufungana.
Msuva amesema kuwa nia yao ni kusonga mbele kwa hiyo wamejipanga kwenda kupata matokeo ya ushindi ugenini.
“Hakuna kinachoshindikana kwenye mpira, kama wao walivyoweza kupata sare ndivyo na sisi tutakavyo pata matokeo ya ushindi ugenini,” alisema Msuva.