Conte, Mourinho kuvaana FA England

Muktasari:

  • Manchester wametinga hatua ya fainali baada ya kuifunga Tottenham Hotspur mabao 2-1 mechi ya nusu fainali jana jumamosi.

KIKOSI cha Chelsea kilicho chini ya kocha Antonio Conte kimetinga hatua ya fainali ya Kombe la Ligi (FA) baada ya kuifunga Southampton mabao 2-0, sasa watavaana na Manchester United.

Chelsea imefunga mabao hayo kupitia kwa Olivier Giroud dakika ya 46, baada ya kupokea pasi kutoka kwa Eden Hazard na Alvaro Morata dakika ya 82, akipokea pasi kutoka kwa Cesar Azpilicueta.

Morata alifunga bao hilo la pili akitokea benchi kuchukua nafasi ya Oliver  na akapachika bao hilo dakika mbili tu  baada ya kuingia.

Chelsea watacheza fainali katika uwanja huo wa Wemble ambao waliwafunga Southampton na Manchester United ya Jose Morinho.

Manchester wametinga hatua ya fainali baada ya kuifunga Tottenham Hotspur mabao 2-1 mechi ya nusu fainali jana jumamosi.