Chelsea yafikia makubaliano binafsi na Sandro wa Juventus

Muktasari:

  • Beki huyo wa Juventus atajiunga na Stamford Bridge kwa gharama ya pauni 60milioni baada ya Chelsea kuonyesha nia ya kumtaka.
  • Baada ya ofa ya pauni 45milioni iliyokataliwa na  Juve 'Old Lady', sasa kocha Antonio Conte yuko tayari kuja na dau jipya.

London, England. Beki wa Juventus, Alex Sandro amefikia makubaliano binafsi na Chelsea na sasa wakati wowote atajiunga  Stamford Bridge.

Beki huyo wa Juventus atajiunga na Stamford Bridge kwa gharama ya pauni 60milioni baada ya Chelsea kuonyesha nia ya kumtaka.

Baada ya ofa ya pauni 45milioni iliyokataliwa na  Juve 'Old Lady', sasa kocha Antonio Conte yuko tayari kuja na dau jipya.

Kwa mujibu wa gazeti la Italia, Corriere delle Sera, Mbrazili huyo mwenye miaka 26, anahamu kubwa ya kuhamia London, lakini kama mabingwa hao wa Serie A watakuwa tayari kupokea pauni60milioni.

CalcioMercato awamedai kuwa Sandro amehaidiwa mshahara wa pauni 6milioni kwa mwaka endapo atasaini Chelsea, hasa baada ya kukataa kusaini mkataba mpya Juventus.

Taarifa zinadai miamba hiyo ya Italia tayari imeshaanza kuangalia wachezaji wa kuziba pengo lake ambao ni Benjamin Mendy wa Monaco, pamoja na Matteo Darmian wa Manchester United.

London, England. Beki wa Juventus, Alex Sandro amefikia makubaliano binafsi na Chelsea na sasa wakati wowote atajiunga  Stamford Bridge.

Beki huyo wa Juventus atajiunga na Stamford Bridge kwa gharama ya pauni 60milioni baada ya Chelsea kuonyesha nia ya kumtaka.

Baada ya ofa ya pauni 45milioni iliyokataliwa na  Juve 'Old Lady', sasa kocha Antonio Conte yuko tayari kuja na dau jipya.

Kwa mujibu wa gazeti la Italia, Corriere delle Sera, Mbrazili huyo mwenye miaka 26, anahamu kubwa ya kuhamia London, lakini kama mabingwa hao wa Serie A watakuwa tayari kupokea pauni60milioni.

CalcioMercato awamedai kuwa Sandro amehaidiwa mshahara wa pauni 6milioni kwa mwaka endapo atasaini Chelsea, hasa baada ya kukataa kusaini mkataba mpya Juventus.

Taarifa zinadai miamba hiyo ya Italia tayari imeshaanza kuangalia wachezaji wa kuziba pengo lake ambao ni Benjamin Mendy wa Monaco, pamoja na Matteo Darmian wa Manchester United.