Chelsea kwa Barca, Real na PSG hapatoshi
Muktasari:
Mechi za mtoano zitafanyika kuanzia Februari mwakani ikiwa ni hatua ya mtoano
Nyon, Uswisi. Chelsea imetupwa kwa Barcelona katika hatua 16 bora ya Ligi ya Mabingwa, wakati mabingwa watetezi Real Madrid wakipagwa kwa Paris-St-Germain.
Manchester City imepewa wapinzani dhaifu kidogo kulinganisha na wenzake katika Ligi Kuu England ikipangwa kucheza dhidi ya mabingwa wa Uswisi, Basel.
Manchester United inakupushia fainali ya msimu uliopita Europa Ligi kwa kupangwa dhidi ya Sevilla itaanza mechi yake ugenini.
Tottenham watakuwa na kibarua kizito ugenini wakati watakapowavaa Juventus, wakati Liverpool wataonyeshana kazi na Porto katika ratiba hiyo iliyopagwa Nyon.
Japokuwa kwa sasa mashabiki Chelsea hawana wasiwasi sana, pamoja na kipigo cha mwishoni mwa wiki kutoka kwa West Ham, lakini wanajivunia rekodi nzuri dhidi ya Barcelona inawabeba.
Nyota wa miamba hiyo ya Catalan, Lionel Messi hajawahi kufunga dhidi ya Chelsea katika michezo nane aliyocheza dhidi ya yao ikiwa ni rekodi mbaya zaidi kwa mshambuliaji huyo.
Ratiba kamili
Juventus vs Tottenham
FC Basel vs Manchester City
FC Porto vs Liverpool
Sevilla vs Manchester United
Real Madrid vs Paris Saint-Germain
FC Shaktar Donetsk vs AS Roma
Chelsea vs Barcelona
Bayern Munich vs Besiktas