Bao la Bale laipeleka Real Madrid nusu fainali

Muktasari:

Real Madrid yatinga nusu fainali Kombe la Dunia la vilabu

Hispania. Real Madrid imeitungua mabao 2-1 klabu ya Al Jazira na bao la Greth Bale lilitosha kuipeleka timu yake kwenye nusu fainali ya Kombe la Dunia kwa vilabu.

Bahati ya mtende ilikuwa kwa Bale, baada ya kugusa mpira mara ya kwanza na hakufanya makosa kutokana ana kuiandikia Madrid bao la ushindi dakika ya 81.

Awali, Cristiano Ronaldo aliisawazishia timu yake bao dakika ya 53 ikiwa ni siku chache zimepita tangu aliposherehekea tuzo yake ya Ballon d’Or kwa mara ya tano.