#WC2018: Kylian Mbappe ashinda tuzo ya mchezaji bora wa Kombe la Dunia 2018.

Kiungo wa Ufaransa na Paris Saint-Germain, Kylian Mbappe.

Muktasari:

Licha ya kuvunja rekodi nne kwenye michuano hii, ikiwa ni pamoja tuzo ya mchezaji mwenye umri mdogo kuwahi kucheza kombe la dunia, rekodi ya kinda aliyewahi kufunga mabao mawili kwenye Kombe la Dunia, rekodi ya kinda aliyefunga kwenye mechi ya fainali na rekodi ya kutwaa kombe, Mbappe ndiye mchezaji bora wa mashindano haya.

Moscow, Russia. Nyota imemuwakia. Hiyo ndio kauli unayoweza kutumia unapomzungumzia kiungo wa Ufaransa na Paris Saint-Germain, Kylian Mbappe, baada kutangazwa kuwa ndiye mshindi wa tuzo ya mchezaji bora chipukizi katika fainali Kombe la Dunia 2018.

Licha ya kuvunja rekodi nne kwenye michuano hii, ikiwa ni pamoja tuzo ya mchezaji mwenye umri mdogo kuwahi kucheza kombe la dunia, rekodi ya kinda aliyewahi kufunga mabao mawili kwenye Kombe la Dunia, rekodi ya kinda aliyefunga kwenye mechi ya fainali na rekodi ya kutwaa kombe, Mbappe ndiye mchezaji bora wa mashindano haya.

Mbappe amekuwa mchezaji wa pili wa Ufaransa kuwahi kushinda tuzo hiyo, baada ya Paul Pogba aliyeshinda tuzo hiyo miaka minne iliyopita. Tuzo hiyo inaweza ikashindwa na mchezaji aliyezaliwa na baada ya Januari mosi.

Kigezo kingine kinachotumiwa kupata mshindi wa tuzo hiyo ni ufundi uwanjani, kasi, utundu udambwidambwi, mchango kikosoni na uungwana mchezoni, kwa mujibu wa kamati ya ufundi ya FIFA. Mbappe amefunga mabao manne kwenye michuano hii, ikiwemo bao la nne, katika ushindi walioupata kwenye fainali dhidi ya Croatia.