IMBA NA MWANASPOTI: Wimbo ‘Sitabaki Nilivyo’ unavyowatoa machozi wengi

Wimbo huo umeimbwa na msaani wa muziki wa Injili, Joel Lwanga na kurudiwa na kufanyiwa ‘cover’ na wasanii mbalimbali  na kutuma kwenye kurasa za mitandao ya kijamii.
Miongoni mwa wasanii waliourudia ‘cover’ ni Lulu Maiko lakini pia marehemu mtoto Patrick Peter aliwahi kuufanyia ‘cover’ akionyesha kuupenda wimbo huo.
Maisha haya, ninapita tu
Hali hii ya sasa ni kwa muda tu
Ushindi wangu, U karibu nami
Mtetezi wangu, yu hai .

Sitabaki kama nilivyo
Silalamiki, wala sikufuru
Najua ni darasa napitishwa
Imani yangu ipo kwenye kipimo .

Najua nitapita tu
Sitamani za wengine wala sijilinganishi
Najua wakati wangu upo
Siogopeswhi na mapito ninayoyapitia
Namwamini yule aliyeruhusu nipite .

Mtetezi wangu
Yu hai (Yu hai)
Sitabaki kama nilivyo………

Wimbo huo umeombwa na Cecilia Elius wa Chanika mkoani Dar es Salaam umwendee rafiki yake Christiner Joseph