Nakuru: Baada ya kusaini mikataba mipya na Simba, straika wa zamani wa Tanzania
Prisons, Mohammed Rashid na winga, Shiza Kichuya wanatarajiwa kuwasili mjini hapa leo Jumapili ili kuongeza nguvu.
Rashid aliyefunga mabao 10 msimu uliopita, amejiunga na Simba kwa mkataba wa miaka
mitatu wakati Kichuya amesaini mkataba mpya wa miaka miwili wa kuendelea kuitumikia timu
hiyo aliyoshinda nayo taji moja la FA na Ligi Kuu katika miaka yake miwili ya mwanzo.
Meneja wa Simba, Richard Robert alisema Kichuya na Rashid watawasili sambamba na
Mzamiru Yassin kwaajili ya kuwabeba kwenye mechi za michuano ya SportPesa.
“Tuna wachezaji 14 hapa hivyo wakiwasili hao watafika 17, wanatosha kwa michuano hii,
tunapaswa kuwaamini tu ili wafanye kazi,” amesema Richard.