LONDON, ENGLAND
MSHAMBULIAJI wa Manchester United, Wayne Rooney atasaini mkataba wa mpya katika klabu yake wenye thamani ya pauni milioni 35 (sawa na shilingi bilioni 70 za Tanzania). Mkataba huo utamfanya nyota huyo akae Manchester United mpaka mwaka 2015.
Rooney atakuwa nyota anayelipwa zaidi Manchester United ambapo atakuwa akipata pauni 130,000 kwa wiki. Na imeelezwa kuwa mchezaji huyo atasaini mkataba huo kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu England.
Mkurugenzi wa Manchester United, David Gill atakaa na Rooney na wawakilishi wake baada ya mchezaji huyo kutoka Barbados, ambapo amekwenda kwa ajili ya mapumziko.
Ingawa Rooney hana mpango wa kuondoka Manchester United, viongozi wa Old Trafford, wanataka nyota huyo aongeze mkataba wa muda mrefu, ambao utasaidia kuziweka mbali klabu nyingine zinazomtamani.
Mazungumzo ya mkataba mpya kwa mchezaji huyo yalichelewa kutokana na kusubiri kumalizika kwa fainali za Kombe la Dunia.
Rooney, amekuwa akilipwa pauni 90,000 kwa wiki nyuma Rio Ferdinand anayelipwa pauni 120,000 kwa wiki.