SI Tanzania tu ambako kuna makomandoo wanaouuza tiketi za magendo za kuingilia uwanjani, hata Sauzi wapo.
Polisi jijini hapa wanamshikilia kijana mmoja kwa kuuza tiketi za kuingilia katika mechi ya Brazil na Korea Kaskazini kwenye Uwanja wa Ellis Park juzi Jumanne.
Brigedia Sally de Beer alisema jana kuwa kijana huyo alikamatwa juzi Jumanne jioni akiuza tiketi za mechi hiyo nje ya Uwanja wa Ellis Park.
Alisema bado wanaendelea kumshikilia kijana huyo huku wakifanya uchunguzi zaidi wa matukio ya uuzwaji wa tiketi ambazo zimetapakaa katika viwanja mbalimbali.
Mechi ya Brazil na Korea Kaskazini ilikuwa ni miongoni mwa mechi ya kuvutia, licha ya kuwa mashabiki walikuwa katika wakati mgumu
kutokana na baridi kali jijini hapa.Mamlaka ya hali ya hewa ilitoa taarifa kuwa hali ya hewa
ilikuwa 2C.