FANYENI kama mama yenu alivyokuwa akiwaambia kila mara, makocha wa Ujerumani wamekuwa wakiwaambia wachezaji wakati wakijiandaa kuhakikisha kuwa baridi haiwaathiri katika mechi yao ya kesho Ijumaa dhidi ya Serbia.
"Wachezaji wote hawana budi kufuata aina ya ushauri mliokuwa wakipewa na mama zenu. Kausha nywele baada ya kuoga na kila mara vaeni nguo za joto," alisema kocha msaidizi Hansi Flick alipoongea na waandishi wa habari.
Hali ya baridi kali kwenye kambi yao iliyo Erasmia karibu na Pretoria imeshamuathiri mmoja baada ya kiungo Bastian Schweinsteigerkulazimika kufanya mazoezi peke yake ili akabiliane na baridi.
Hata hivyo, atakuwa fiti kucheza mechi ya pili dhidi ya Serbia.
"Atafanya mazoezi ya pekee ili atoke jasho kidogo ili aweze kufanya mazoezi na wenzake tena kesho," alisema Flick.