Sep 5, 2010, 11:43 am TFF UEFA FIFA Yahoo Sport CAF Staff Mail Premier League English News Spoti Majuu
 
 
 
 
 
 
 
 

 

Imewekwa:: 2010-06-17 11:21:00
Amuomba radhi Naibu Waziri
KIUNGO wa Ghana, Laryea Kingston amemuomba radhi Naibu Waziri wa Michezo, Nii Nortey Dua kutokana na kauli zilizotolewa na mama yake (Laryea).

Mama yake anadaiwa kumrushia matusi naibu waziri huyo baada ya Kingston kutemwa kwenye kikosi cha wachezaji 23 walioenda Afrika Kusini kwenye fainali za Kombe la Dunia.

Akizungumza na tovuti ya Joy Sports, Waziri huyo alisema kuwa alipigiwa simu na Kingston wakati timu ikiwa kambini Scotland na akaomba radhi.

Nii Nortey Dua, ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Ledzorkuku alielezea kuwa tukio hilo ni la kawaida katika kazi yake.

"Nilishasahau suala hilo hata kabla ya kupigiwa simu," alisema.
Kingston alikulia kwenye jimbo hilo hadi alipoanza kucheza soka la kulipwa nje ya nchi.
Toa Maoni Chapisha(Print) Facebook Tuma kwa rafiki
Habari Zingine
Wabongo wamrudisha Mariga Dar
Rage aidai Mwanaspoti Sh. bilioni moja
Jabulani kumi zaisisimua Simba
Kipa Yanga aingilia anga za Kaseja
Mafowadi 11 watibuana Mtibwa Sugar
Taswa wajadiliana na Mkurugenzi wa Michezo
Mafisango aguna, aipa tano Azam
Mwingereza aanza kazi Zanzibar
Simba yaipeleka Yanga Kirumba
Poulsen ampiga tafu Phiri Simba
 
 
 
 
 
© Mwananchi Communications Ltd:2007-2010:Started October 1,2007http://www.mwanaspoti.co.tz/readnewzt_sp.php?id=4224