LAGOS, NIGERIA
MWANAMUZIKI Muma Gee wa Nigeria ameibuka na 'kuruka kimanga' kwamba hana uhusiano wa kimapenzi na muigizaji wa Nollywood, Emeke Ike na kwamba hafikirii kama kuna siku atamtamani mwanaume huyo.
Hata hivyo Muma Gee alionekana kuwa karibu na muigizaji huyo katika mashindano ya Nyota wa Nigeria yaliyoitwa Gulder Ultimate Search, ambayo yalimalizika hivi karibuni na kuhusu hilo Muma Gee alisema:
"Nilikuwa karibu na Emeke kwa kuwa niliona ni mtu mwenye busara katika kundi hilo. Niliona kwamba ni mtu ambaye angalau alikuwa na hadhi yangu.
"Nilifahamiana na Emeka Ike kabla ya mashindano hayo kwa hiyo sikuona sababu ya kuwa mbali naye. Nilikaa katika mashindano kwa siku kadhaa, familia yangu haikuwepo, ilibidi kuwa na mtu wa kuzungumza naye.
Lakini cha kushangaza ni kwamba watu walianza maneno kwamba nilikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanaume huyo jambo ambalo si ukweli.
"Watu wanatakiwa kuwa na upeo wa kutofautisha urafiki wa kawaida na mapenzi."
Na kuhusu habari kwamba waliwahi kufanya mapenzi bafuni dada huyo alisema: "Siwezi kufanya jambo kama hilo kwa kuwa najiheshimu mwenyewe vilevile namheshimu Emeke na mke wake.