Sep 5, 2010, 11:59 am TFF UEFA FIFA Yahoo Sport CAF Staff Mail Premier League English News Spoti Majuu
 
 
 
 
 
 
 
 

 

Imewekwa:: 2010-06-08 09:47:00
Mosunmola Filani apigwa mkwara
LAGOS, NIGERIA
MOSUNMOLA Filani ni mmoja wa wadau wakubwa wa filamu nchini Nigeria kutokana na juhudi zake katika uandaaji na uigizaji wa filamu, lakini tatizo la dada huyo ni moja tu, wizi wa wanaume za watu.
Na safari hii dada huyo amekuwa na uhusiano na Muyiwa Ademola, ambaye ni mwanaume aliyeoa. Lakini amekwaa kisiki kwa kuwa mke wa Muyiwa amekujaa juu na kumwambia dada huyo achague moja; amuache mwanaume huyo au apotezwe mjini.
Mke wa Muyiwa ametuma ujumbe kwamba ameandaa adhabu kali kwa muigizaji huyo na iwapo adhabu hiyo ikimshukia ni wazi kwamba atahama mjini.
Dada huyo amesema kwamba ameandaa tindikali kwa ajili ya kumjeruhi Mosunmola na kumfanyia mambo mengine ya kihuni kama ataendelea kutembea na mume wake.
Na imefahamika kwamba ujumbe huo umekuwa sumu kali kwa Mosunmola ambaye sasa ameanza kumuogopa Muyiwi kama ukoma.
Toa Maoni Chapisha(Print) Facebook Tuma kwa rafiki
Habari Zingine
Wabongo wamrudisha Mariga Dar
Rage aidai Mwanaspoti Sh. bilioni moja
Jabulani kumi zaisisimua Simba
Kipa Yanga aingilia anga za Kaseja
Mafowadi 11 watibuana Mtibwa Sugar
Taswa wajadiliana na Mkurugenzi wa Michezo
Mafisango aguna, aipa tano Azam
Mwingereza aanza kazi Zanzibar
Simba yaipeleka Yanga Kirumba
Poulsen ampiga tafu Phiri Simba
 
 
 
 
 
© Mwananchi Communications Ltd:2007-2010:Started October 1,2007http://www.mwanaspoti.co.tz/readnewzt_sp.php?id=4180