LONDON, ENGLAND
HUKU kikosi cha England kikijiandaa kutua Afrika Kusini kwa ajili ya fainali za Kombe la Dunia, Frank Lampard anaonekana kuwa na wakati mgumu kukubaliana na ukweli kuwa atalazimika kuwa mbali na mpenzi wake Christine Bleakley kwa wiki kadhaa.
Na Lampard anafahamu 'mkwara' wa kocha wa England, Fabio Capello ambaye amebainisha kwamba hataki kuona wapenzi, wala wake wa wachezaji katika kambi yake nchini Afrika Kusini.
Katikati ya wiki hii Lampard na dada huyo walikuwa wakionekana pamoja mara kwa mara jambo ambalo limetafsiriwa kwamba walikuwa wanaagana.
Lakini ingawa kocha wa England amesema wachezaji wake hawataruhusiwa kuonana na wapenzi wao katika kipindi chote cha mashindano, wanawake hao wamesaka hoteli za karibu na watahudhuria mechi mbalimbali. England inatarajia kukwaana na Japan, kesho Jumapili huko Austria katika mechi ya maandalizi.