LONDON, ENGLAND
WAYNE Rooney ametoa onyo kwa Cristiano Ronaldo kuwa 'atamfunika' katika Fainali za Kombe la Dunia mwezi ujao kwa kuwa dalili zimeonekana mapema.
Wachezaji hao walitumia muda saa kadhaa kucheza 'gemu' katika kompyuta ambapo Rooney alimshinda mpinzani wake.
Rooney mwenye miaka 24 anaamini atampiku Cristiano mwenye miaka 25 katika fainali hizo kwa kuwa nuru njema imeanza kuonekana.
Ingawa Wayne na mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United wapo katika timu tofauti wamekuwa wakiwasiliana mara kwa mara na wamekuwa akicheza gemu za video katika mtandao.
Mtu mmoja kutoka Manchester United alisema: "Wayne anaweza sana kucheza 'video game' kama anavyokuwa uwanjani Old Trafford.
"Huwa anafanya vema bila kujali anaangaliwa na watu 80,000 au yupo peke yake chumbani."