Sep 5, 2010, 12:35 pm TFF UEFA FIFA Yahoo Sport CAF Staff Mail Premier League English News Spoti Majuu
 
 
 
 
 
 
 
 

 

Imewekwa:: 2010-05-22 14:05:00
Chelsea
BAADA ya mafanikio ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa England na Kombe la FA, nyota mbalimbali wa Chelsea wanajipanga kujiunga na timu zao za taifa kwa ajili ya fainali ya Kombe la Dunia.

Habari njema ni kuwa staa wa Chelsea na Ghana, Michael Essien anaendelea vizuri na anafanya mazoezi maalumu kwenye uwanja wa mazoezi wa Chelsea ulioko Cobham.

Essien ameiamba tovuti ya klabu yake kuwa anaendelea vizuri na hivi karibuni alikutana na viongozi wa Shirikisho la soka Ghana kuongelea maandalizi ya Kombe la Dunia.
Amesema kwa sasa hataki kujipa presha ya kujiunga na timu ya Ghana lakini anachotaka ni kupona vizuri.

Essien amedokeza watu wengi wa Ghana wamekuwa wakiwasiliana naye na kumwombea ili acheze kwenye fainali za Kombe la Dunia.

Essien amesema ana matumaini ya kucheza fainali za Kombe la Dunia lakini bado anajisikilizia.

Amedai kitu muhinu ni kuwa fiti kwanza kutokana na kuwa hajacheza soka tangu Januari.
Toa Maoni Chapisha(Print) Facebook Tuma kwa rafiki
Habari Zingine
Wabongo wamrudisha Mariga Dar
Rage aidai Mwanaspoti Sh. bilioni moja
Jabulani kumi zaisisimua Simba
Kipa Yanga aingilia anga za Kaseja
Mafowadi 11 watibuana Mtibwa Sugar
Taswa wajadiliana na Mkurugenzi wa Michezo
Mafisango aguna, aipa tano Azam
Mwingereza aanza kazi Zanzibar
Simba yaipeleka Yanga Kirumba
Poulsen ampiga tafu Phiri Simba
 
 
 
 
 
© Mwananchi Communications Ltd:2007-2010:Started October 1,2007http://www.mwanaspoti.co.tz/readnewzt_sp.php?id=4086