KUNA maandalizi kamambe ya msimu ujao na Manchester United imejipanga kucheza mechi za kirafiki Marekani na Canada, kwa mujibu wa Ofisa Mkuu Mtendaji wa klabu hiyo, David Gill.
Akizungumza katika uzinduzi wa ziara hiyo jijini New York, Gill amesema wamepania kufanya vizuri msimu ujao na anaamini ziara hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa timu hiyo.
"Ziara hizi zinasaidia kusogeza klabu karibu na wapenzi wao," aliongeza Gill, ambaye timu yake imevuliwa ubingwa na Chelsea.
"Unajua ziara kama hizi zinaongeza mashabiki na pia ni nafasi kwa wadhamini wetu kujitangaza.
Gill amesema ziara hiyo itaiweka timu hiyo vizuri kwa ajili ya msimu ujao.
Alisema pia wanapenda kwenda Marekani kwa kuwa viwanja vya huko viko kwenye hali nzuri.