Sep 9, 2010, 9:43 am TFF UEFA FIFA Yahoo Sport CAF Staff Mail Premier League English News Spoti Majuu
 
 
 
 
 
 
 
 

 

Imewekwa:: 2010-03-06 04:48:00
Prisons, Toto roho mkononi
OLIVER ALBERT

OSWARD Morris wa Prisons amewaambia wenzake: "Komaeni tuifunge Toto African kwani mechi hii ndio itakayoamua maisha yetu.'

Prisons inashuka kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza leo Jumamosi kuivaa Toto African katika mchezo unaokutanisha timu zilizo katika hatari ya kushuka daraja.

Morris, ambaye ameichezea Prisons kwa miaka 14, alisema mchezo huo ni kama wa fainali na kwani ndio utatoa mustakabali wao wa kubaki kwenye ligi.

"Tukiishinda Toto African tutajiweka pazuri na tutapanga mikakati madhubuti ya kuhakikisha tunashinda mechi zote zilizobaki, lakini tukifungwa hali itakuwa ngumu."

Prisons ikishinda itafikisha pointi 20 na itasalia na mechi tatu, ambazo ikishinda itamaliza ligi na pointi 29 wakati Toto African inayokamata mkia ikiwa na pointi 13 ikiibuka na ushindi itakuwa na pointi 16, nayo itabakiza mechi tatu.
Toa Maoni Chapisha(Print) Facebook Tuma kwa rafiki
Habari Zingine
Phiri hana shida, Mgosi, Kanoni waibukia Tanga
Mkenya aipa Simba mambo mawili
Henry arudi Norway majeruhi
Kiungo Yanga mambo mazuri
Mafisango atunisha msuli,aigunia Simba Tanga
Humoud azua tafrani Simba
Wabongo wamrudisha Mariga Dar
Rage aidai Mwanaspoti Sh. bilioni moja
Jabulani kumi zaisisimua Simba
Kipa Yanga aingilia anga za Kaseja
 
 
 
 
 
© Mwananchi Communications Ltd:2007-2010:Started October 1,2007http://www.mwanaspoti.co.tz/readnewzt_sp.php?id=3620