Sep 9, 2010, 8:59 am TFF UEFA FIFA Yahoo Sport CAF Staff Mail Premier League English News Spoti Majuu
 
 
 
 
 
 
 
 

 

Imewekwa:: 2010-02-06 03:45:00
Henry Joseph kamili gado
Na Michael Momburi

HENRY Joseph anayeichezea Kongsvinger ya Norway amesema kuwa yupo fiti tayari kwa Ligi Kuu ya nchi hiyo inayoanza mwezi Machi.

Mchezaji huyo wa zamani wa Simba aliiambia Mwanaspoti kwa njia ya simu jana kuwa kila kitu kinaenda safi na ameshakuwa fiti asilimia mia moja.

"Nafanya mazoezi sana na maumivu ya mbavu yaliyokuwa yananikabili yameshakwisha kama wiki mbili au tatu zilizopita na madaktari wamesema niko salama kwa shughuli,"alisema Henry aliyezaliwa miaka 25 iliyopita jijini Mwanza, Tanzania.

"Sasa hivi najinoa sana nataka niwe fiti kwa mechi za kirafiki ambazo zinaanza wiki ijayo na Ligi Kuu ambayo inakuja siku za usoni.

"Ninavyojiona niko vizuri sana na nitafanya vizuri sana kadri inavyowezekana kama sitaumia tena wala kusumbuliwa na tatizo lolote," ambaye, aliibuliwa na Simba kutoka kwenye shule ya sekondari ya Makongo.

Henry aliumia mbavu katika mechi ya kirafiki kwenye uwanja wa Taifa baina ya Taifa Stars na Ivory Coast. Stars ilifungwa bao 1-0 na Didier Drogba anayeichezea Chelsea ya England, ambayo kesho Jumapili inacheza na Arsenal.
Toa Maoni Chapisha(Print) Facebook Tuma kwa rafiki
Habari Zingine
Phiri hana shida, Mgosi, Kanoni waibukia Tanga
Mkenya aipa Simba mambo mawili
Henry arudi Norway majeruhi
Kiungo Yanga mambo mazuri
Mafisango atunisha msuli,aigunia Simba Tanga
Humoud azua tafrani Simba
Wabongo wamrudisha Mariga Dar
Rage aidai Mwanaspoti Sh. bilioni moja
Jabulani kumi zaisisimua Simba
Kipa Yanga aingilia anga za Kaseja
 
 
 
 
 
© Mwananchi Communications Ltd:2007-2010:Started October 1,2007http://www.mwanaspoti.co.tz/readnewzt_sp.php?id=3504