LONDON, England
LICHA ya John Terry kukabiliwa na madai ya kutembea na mke wa Wayne Bridge, Chelsea imesema itampa ushirikiano katika kipindi hiki kigumu.
Habari kutoka Chelsea zinasema mmiliki wa klabu hiyo, Roman Abramovich alimwita Terry na kumwambia klabu ipo pamoja naye katika kipindi hicho kigumu.
Kumekuwa vielelezo vya wazi vinavyothibitisha kwamba Terry alilala na aliyekuwa mke wa Bridge aitwaye Vanessa Perroncel, lakini Abramovich anaona kuwa hakuna sababu ya kumchukulia hatua za kinidhamu mchezaji huyo.
Mtu mmoja wa karibu na Abramovich alisema: "Roman alimwambia John kuwa asiwe na wasiwasi kwani Chelsea haitamtupa katika wakati huo mgumu.
"Nadhani anahitaji kutulizwa katika kipindi hiki kigumu.
"Ukweli ni kwamba Terry hajavunja sheria. Jambo la msingi ni kuhakikisha anashughulikia suala hilo mpaka litakapomalizika.
"Ni mtu anayeheshimika katika kikosi, ni mmoja kati ya wanafamilia wa Chelsea."
Wiki hii, Terry alifanya mazoezi na wachezaji wenzake kama kawaida na hali ilikuwa shwari uwanjani, hakukuwa na minong'ono yoyote.