Jul 30, 2010, 2:41 pm TFF UEFA FIFA Yahoo Sport CAF Staff Mail Premier League English News Spoti Majuu
 
 
 
 
 
 
 
 

 

Imewekwa:: 2009-10-19 18:20:00
Kikosi chamchefua Ancelotti
Carlo
LONDON, England
KOCHA wa Chelsea, Carlo Ancelotti amesema kikosi chake kinatakiwa kujiimarisha vema ili kuepuka kipigo kingine.

Timu hiyo ilichapwa mabao 2-1 na Aston Villa huku wauaji wakiwa Richard Dunne na James Collins. Bao la kwanza la Chelsea lilifungwa na Didier Drogba.

"Tumekosa amani kwa sababu tulicheza vema na kupoteza mchezo, hatukuwa na sababu ya kupoteza mechi hiyo," alisema Ancelotti.

"Mtu huwezi kupata maumivu makali kama timu yako imecheza chini ya kiwango na kufungwa, Villa walijitahidi, lakini kiwango cha Chelsea kilikuwa kikubwa zaidi.”

"Katika mechi zinazokuja tunatakiwa kujituma zaidi, naamini jitihada kubwa huzaa matunda mazuri.”

"Tulipofungwa, tuliumia sana, lakini baada ya muda kidogo wachezaji walisahau maumivu na kufikiria mechi nyingine," alisema.
Toa Maoni Chapisha(Print) Facebook Tuma kwa rafiki
Habari Zingine
Kocha Profesa wa Serbia atua Simba
Njoroge avaa bomu, Papic ategua
Okwi azuiwa kufanya mazoezi ya Mziray
Mghana Yanga amuwinda Mgosi
Papic atajwa kurudi Afrika Kusini
Mbrazili Azam aleta vita
Henry Joseph chupuchupu
Razak Khalfan atamba Marekani
Orlando Pirates yainoa Yanga
Saa mbili za jasho na damu Yanga
 
 
 
 
 
© Mwananchi Communications Ltd:2007-2010:Started October 1,2007http://www.mwanaspoti.co.tz/readnewzt_sp.php?id=2701