LONDON, England
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kwamba mchezaji Andrey Arshavin wa Russia ni hazina kwa klabu.
Arshavin amekuwa akijiweka fiti tangu alipojiunga na kikosi hicho katika dirisha dogo la usajili wa mwezi Januari.
Imeonekana kwamba mshambuliaji huyo ameanza kukaa sawa baada ya kupachika mabao mawili wakati timu yake ilipotoka kifua mbele kwa mabao 4-0 dhidi ya Blackburn Rovers.
Wenger alisema: "Alicheza kwa juhudi, nadhani hata yeye ameshangazwa na uwezo aliouonyesha.
"Lakini ninadhani kwamba ni mtu anayependa changamoto kwa kuwa alidiriki kuondoka St Petersburg, ambako alikuwa nyota na kufika England akiwa na umri wa miaka 28 inaonyesha ana uhakika na anachokifanya.
"Ninapenda wachezaji kama hao kwa sababu katika hatua ya mwisho wanaweza kukusaidia. Nadhani kila mchezaji anatakiwa kuwa na ari kama hiyo mpaka mwisho wa msimu.
"Lakini hata sisi tumewahi kuwauza wachezaji wetu kama Alexander Hleb na Tomas Rosicky,ambao walikuwa na miaka kati ya 27 na 30, waliamini kwamba wanaweza kufanya vema mbele ya safari.