Jamani tunakuombeni hizi habari zilizomo katika gazeti ili ni za zazamani na zHabari Hiziinachafuwa roho. Wakati huu tuliokuwa nao kuna mambo mengi na muhimu yanayotokea nchini kwetu hasa zile zinazohusu uasajili wa wachezaji wapya na kutemwa baadhi ya wengine jambo ambalo wengi sana tuna hamu kuyajuwa
kwa mtoa gazetu la mwanaspoti hili gazetu lenu ni zuri lakini mpaka sasa gazeti hili halitupi matukio ya kila siku ya kichezo kwani mpaka sasa gazeti hili linaonyesha habari za tarehe 24/05/2010 na sasa leo ni tarehe 05/06/2010 jaribu kuliweka katika hali ya kupata habari mpya kila siku.
stars amueni moja ama Brazil au CHAN hivyo chezeni kufa na pona dhidi ya Rwanda huku ikiwezekana kupata majerui na kushindwa kuwakabili Brazil au chezeni kizembe na Rwanda ili muuze sura mbele ya Brazil. Kama ni wazalendo kweli basi mtashinda Rwanda na yeyote ambaye atakuwa fiti atacheza dhidi ya Brazil. CHAN ni bora kuliko mechi yoyote ya kirafiki hata kama ni kucheza na timu kutoka mbinguni. Pangeni na mchague.
Inasikitisha sana kuona TFF ikipanga viingilio vikubwa kwenye mechi zinazochezwa hapa nchini kiasi cha kuwakatili watanzania wa kawaida kushindwa kuingia uwanjani kuangalia mechi. Viingilio vilivyopangwa kwa ajili ya mechi ya Tanzania na Brazili ni vya kibepari TFF waache kujali matumbo yao na kuwasahau watanzania maskini
Ujaji wa timu ya taifa ya Brazil hapa Tanzania kucheza na wenyeji (taifa stars) italeta changamoto kubwa kwa timu yetu ya taifa kupata mwangaza wa kushiriki kombe la dunia miaka ya mbele. Hivyo nawaomba wachezaji wa taifa stars wakaze buti kuichapa Brazil ili ijulikanwe zaidi kisoka ulimwenguni kwa kuwachapa mabingwa hao mara tano wa kombe la dunia.