Zari ampiga stop mtoto wa Hamisa urafiki wa Istagram

Muktasari:

  • Hamisa aliandika "Am praying for twins now. Inshallah (a girl & a boy) would be perfect "

Jana imetokea vita kali katika mtandao wa Snapchat huku Hamisa na Zari wakitupiana vijembe vya hapa na pale huku mwenza huyo wa Diamond akimshutumu mtoto wa Hamisa kwa kumfollow mwanaye Instagram.

Hamisa aliandika "Am praying for twins now. Inshallah (a girl & a boy) would be perfect "

Tena akaandika, "Waambie walopanga…mwenye nyumba kaja ndani… ana meremeta.

Baadae tena akaweka picha ya gari huku ikisindikizwa na maneno ya "Dee Platnumz".

Baadaye akaandika "Na kama kuna mwanamke mwingine unampenda zaidi yangu… basi mwambie mzaa chema shikamoo."

Upande wa Zari yeye alishutumu vikali baada ya hatua ya mtoto wa Hamisa katika Instagram kumfollow mtoto Tiffah kwa kuandika "Laki 2 stop following my kids lol.  Your Obsession needs a mental institution. Like the hell? "

Mara akaweka neno "Yani" likifuatiwa na emoji za kicheko.