Wazaramo waliamsha dude Zanzibar
Muktasari:
Kikundi hicho ambacho kilianzishwa zaidi ya miaka kumi iliyopita,kimesema hakuna vikundi viwili vya Segere kama baadhi ya watu wanavyodhani, ila kuna Segere na Young Star ya Siza Mogela ndio wanadhani ni Segere nyingine.
Zanzibar. Kikundi cha ngoma za asili ya Kizaramo kutoka Tanzania, Segere Original wameweza kuamsha furaha kwa mashabiki zao kwa kutoa burudani ya muziki wa asili unaofanywa na kikundi hicho katika Tamasha la Sauti za busara 2018
Kikundi hicho ambacho kilianzishwa zaidi ya miaka kumi iliyopita,kimesema hakuna vikundi viwili vya Segere kama baadhi ya watu wanavyodhani, ila kuna Segere na Young Star ya Siza Mogela ndio wanadhani ni Segere nyingine.
Aidha walifafanua zaidi kwa kusema, neno Segere limetokana na wimbo waliowahi kuuimba hapo nyuma hivyo wakaona bora walitumie liwe jina la kundi.
Wakati huo huo kundi hilo limeweza kumtambulisha kijana wao mdogo anayefanya muziki wa Singeli aitwaye Elisha Dafa maarufu kama Dogo Elisha.