Irene sasa ameamua kabisa aisee

Irene Paul

MWIGIZAJI, Irene Paul, amedai kuachana na kazi ya utangazaji baada ya kubaini filamu inamlipa zaidi na kumpa fursa ya kufanya mambo makubwa. ìKwangu mimi filamu inanilipa, ndiyo maana nimeachana na kazi nyingine zote ili niwe makini na kazi ya uigizaji. Hapa ninayaona maslahi moja kwa moja," alisema. "Pia filamu imenikutanisha na watu mbalimbali, pia imebadilisha maisha yangu napata ninachohitaji bila wasi wasi." Irene aliyewahi kufanya kazi na vituo vya luninga vya C2C na Clouds TV vya Dar es Salaam alipewa nafasi na Ray kwenye uigizaji na kufanya vizuri. Msanii huyo ameshiriki filamu na wakongwe katika tasnia wakiwamo Steven Kanumba (marehemu sasa). Filamu alizoigiza ni 'I Hate My Birthday', 'Kibajaji', 'More Than Pain' na 'Kalunde' aliyoitengeneza mwenyewe.