Mpigambizi wa Taifa aanza kazi

Muktasari:

Hilal aliondoka nchini juzi baada ya Shirikisho la Kuogelea la Kimataifa (Fina) kumpa ofa ya mafunzo ya mwaka mmoja kutokana na kuwa mwogeleaji pekee wa Tanzania aliyefanya vizuri kwenye michezo ya Olimpiki ya Rio 2016, nchini Brazil.


Dar es Salaam. Mwogeleaji wa timu ya taifa, Hilal Hemed Hilal ameanza mazoezi ya mwaka mmoja kwenye kituo cha kimataifa cha kuogelea cha Thanyapura nchini Thailand huku akipigia hesabu ya medali kwenye michezo ya Jumuiya ya Madola ya mwakani nchini Australia.

 

Hilal aliondoka nchini juzi baada ya Shirikisho la Kuogelea la Kimataifa (Fina) kumpa ofa ya mafunzo ya mwaka mmoja kutokana na kuwa mwogeleaji pekee wa Tanzania aliyefanya vizuri kwenye michezo ya Olimpiki ya Rio 2016, nchini Brazil.