Manji ajiuzuru Yanga

Muktasari:

Kwa mujibu wa barua ya Manji iliyoisaini Mei 22, inasema amejiuzuru uenyekiti na sasa majukumu yote hadi pale uchaguzi mpya utakapofanyika wa kujaza nafasi yake majukumu yote ya timu yatakuwa chini ya Makamu wa Rais, Sanga.

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Yanga, Yussuf Manji ametangaza kujiuzuru uenyekiti wa klabu hiyo kuanzia Mei 20, na majukumu yake kuyaacha kwa makamu wa rais Clement Sanga.

Kwa mujibu wa barua ya Manji iliyoisaini Mei 22, inasema amejiuzuru uenyekiti na sasa majukumu yote hadi pale uchaguzi mpya utakapofanyika wa kujaza nafasi yake majukumu yote ya timu yatakuwa chini ya Makamu wa Rais, Sanga.

Sanga alithibisha kupokea barua ya Manji kujizuru akisema ni kweli nimepokea barua ya mwenyekiti juu ya uamuzi wake wa kupumzika kwa sasa.

Katika barua Manji aliisema huwa kunafikamuda tukiwa tunafuata wito fulani, wakati mimi nikiwa sehemu ya Yanga ilinibidi nijitokeze mbele kwa ajili ya umoja wa klabu yetu tuipendayo na kuongoza. Kulikuwa na wanachama waliokuwa wakigombana, ndipo ilikuwa muda wangu wa kutoa msaada kwa Yanga.

"Sisi sote ni sehemu ya ukoo mkubwa wa Yanga na ukweli mnaufahamu, imani ndiyo jambo ambalo tulilihitaji ndani ya Yanga kuturudisha katika mwelekeo sahihi wa miaka 11 iliyopita."

Taarifa hiyo iliendelea kusema "Kama Mungu alivyotuonyesha kwa kubadili jiwe kuwa mkata, hivyo msaada wangu kwa uwezo wa neema zake, naamini ulifanya mabadiliko chanya na klabu iko imara na huru. Lakini umefikia wakati wangu wa kuachia wengine na wengeni wasifikirie nilikuwa kiongozi aliyetaka cheo chochote au umashuhuri, ila ni upendo uliomgusa kuitumikia Yanga yetu. Pamoja tulifanikiwa mengi sana, na kuandika historia ndani ya Yanga na nilipolea baraka zenu mimi binafsi na familia yanga kupitia furaha japo ndogo, iliyoweza kuwaletea, ambao ninawashukuru sana.

"Nilisema tangu mwaka 2014, kuwa sitagombea katika uchaguzi wa uongozi kwenye nafasi yoyote ndani ya klabu na nikaonyesha mfano kuwa klabu yetu siyo mtu mmoja ila ni yetu sote, na uongozi ni lazima utoke kutoka kwenye kizazi kimoja kwenda kingine.

Iliongeza taarifa hiyo kuwa "Lakini mwaka jana tulikuwa katika mashindano ya mabara na kuacha pengo isingekuwa sahihi, hivyo kinyume na msimamo wangu niligombea uenyekiti wa Yanga na kupata ushindi bila ya kupigwa, lakini kama nikiendelea, nitakuwa ninaonyesha mfano upi kwa watoto wetu ambao wanaipenda Yanga kwa sababu yetu? Kwani Yanga siyo klabu yao kama ilivyokuwa yenu na mimi?"

Muda wangu wa kutangaza kuwa ninakaa pembeni kutoka kwenye nafasi ya mwenyekiti wa Yanga ni sasa, tayari tumekuwa mabingwa wa mashindano tena, tuna kikosi kizuri na wachezaji na makocha, tumeungana kwa umoja haijawahi kutokea, tumerudisha heshima ya kuwa washindano wa ukweli katika klabu Afrika, na kuwa imara zaidi kiuchumi na mkataba wa ufadhili  ya Sportspesa.

Nafahamukuwa bado kuna mengi yanayohitajika kutimizwa, lakini barabar ya mambo yanayotakiwa kutimizwa haiwezi kuisha, na siwezi kuwa mroho wa kuamini kuwa ni mimi pekee nitakayeweza kutufikisha mwisho wa safari.

Muda wangu kama mwenyekiti wa klabu yetu ulikuwa umeongezwa tu na haikumaanisha katika demokrasi yetu uwe ni ule uiokuwa na kikomo.