ABC yausaka ubingwa kikapu
Muktasari:
- Msimu mpya wa RBA umeanza huku Savio wakiwa ni mabingwa watetezi kwa wanaume
Kocha wa ABC, Duruweshi Shamuni ameendelea kutamba na kikosi chake kwa kuifunga UDSM Insider kwa pointi 94-65 katika mchezo wa Ligi ya mpira wa kikapu kanda ya Dar es Salaam (RBA).
ABC imeonekana kuwa moto wa kuotea mbali kwenye msimu huu mpya wa 23 kwa wanaume huku kwa wanawake ukiwa ni wa 21 kwa kupata matokeo ya ushindi katika michezo yao miwili mfululizo.
Kwenye mchezo wao wa kwanza ABC walianza kwa kuifunga Kurasini Heat kwa pointi 71- 42.
“Tulijua namna ya kucheza nao ndiyo maana hawakutupa shida, kuanzia kwenye eneo letu mpaka kwenye eneo lao, uharaka ulitusaidia kwenye kutengeneza mashambulizi yetu,” alisema Duruweshi.
Mchezo mwingine ulichezwa Ijumaa usiku ulishudia Oilers ikichapa Tanzania Prisons kwa pointi 91-57.