Mwasiti wala hamtangazi mpenzi wake

Muktasari:

Alisema lakini anaweza kumtangaza mumewe baada ya kufunga ndoa. Mwasiti aliyasema hayo katika mahojiano na Mwanaspoti jana Jumatano, ambapo pia alifafanua kuhusu uhusiano wake na mtangazaji Sam Missago, akidai wao ni marafiki tu.

MWANAMUZIKI Mwasiti Almas amesema kamwe hawezi kumtangaza mchumba au mpenzi wake hata iweje.
Alisema lakini anaweza kumtangaza mumewe baada ya kufunga ndoa. Mwasiti aliyasema hayo katika mahojiano na Mwanaspoti jana Jumatano, ambapo pia alifafanua kuhusu uhusiano wake na mtangazaji Sam Missago, akidai wao ni marafiki tu.
“Nitasema kuhusu mwandani wangu nikiolewa, siwezi kumtangaza mpenzi au mchumba kwa sasa, hujui ya kesho watu hubadilika, hakuna matata ikiwa nitatangaza mume, kwani sitaathirika lakini mpenzi au mchumba hapana.
Maisha yangu ya mahusiano yanawahusu ndugu jamaa na marafiki na si mashabiki wa muziki wangu, sitaki vitu hivi viingiliane,” alisema Mwasiti.