Abdulrahaman Mussa tatizo lake dogo tu!
Muktasari:
Abdulrahaman anapenda kuvaa jezi namba 17, alicheza katika mechi yao dhidi ya Yanga wakafungwa bao 1-0, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
MASHABIKI wengi wa soka wanajiuliza maswali mengi juu ya kiwango cha mshambuliaji wa Ruvu
Shooting, Abdulrahaman Mussa kuwa kimeshuka, lakini kocha mkuu wa kikosi hicho, Abdulmutik
Haji amefafanua na kusema, majeruhi ndiyo yamesababisha.
Abdulrahman alikuwa moto kwenye safu hiyo ya ushambuliaji msimu uliopita hadi akamaliza akiwa
kinara wa mabao kwenye msimamo wa ligi akifunga 14 sawa na ya Simon Msuva aliyekuwa
anaichezea Yanga.
Kocha huyo amesema: "Ni kweli Abdulrahaman hayuko sawa katika kipindi hiki, hajarudi kwenye
kiwango chake nafikiri yote ni kwa sababu anatoka kwenye majeruhi. Alikuwa mgonjwa na sasa ndiyo
anarudi taratibu."
Abdulrahaman anayependa kuvaa jezi namba 17, alicheza katika mechi yao dhidi ya Yanga
wakafungwa bao 1-0, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.